logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Familia ya Profesa Jay yakanusha madai kuwa amefariki

Aliwambia mashabiki wa Profesa Jay wapuuze madai yanayoenezwa na wambea.

image
na

Yanayojiri18 February 2022 - 05:01

Muhtasari


•Familia ya Mwanamuziki na mwanasiasa mashuhuri kutoka  Tanzania Joseph Haule almaarufu Profesa Jay imekanusha madai kuwa msanii hajafariki.

Mwanamuziki Joseph Haule almaarufu kama Profesa Jay

Familia ya Mwanamuziki na mwanasiasa mashuhuri kutoka  Tanzania Joseph Haule almaarufu Profesa Jay imekanusha madai kuwa msanii huyo amefariki.

Kaka yake Profesa Jay, Black Rhyno akihojiwa na kituo kimoja cha habari, aliwambia mashabiki wa Profesa Jay wapuuza mbali madai yanayoenezwa kwenye mitandao ya kijamii na kuwa  Profesa anaendelea kupata nafuu.

 "Ni uongo. Hajafa. Tuache kusema mambo ambayo si ya kweli,"alisema Kakake Profesa. 

Vilevile mwanasiasa wa Tanzania John Heche alizamia swala hilo ambapo alikana madai hayo akieleza kuwa bado Profesa Jay  afya yake inaendelea kuimarika na hivyo watu wakome kueneza uvumi mbaya.

“Tunakuombea kupona tu ProfessorJayTz hatuna agenda nyingine nawe mtu wa watu Hatusikilizi maombi machafu ya wafuasi wa shetani, Damu ya yesu inanena mema kwako upone haraka,” alisema John Heche.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved