logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Karen Nyamu aibua mdahalo kuhusu ujauzito wake

Akijibu shabiki mmoja aliyezua madai kwamba Samidoh alikana ujauzito wa Nyamu.

image
na

Makala22 February 2022 - 04:52

Muhtasari


• Karen alikuwa akijibu shabiki mmoja aliyezua madai kwamba Samidoh alikana ujauzito wa mwanasiasa huyo.

 

Mwanasiasa Karen Nyamu Picha: RADIO JAMBO

Mwanasiasa na Baby mama wa Samidoh, Karen Nyamu siku ya Jumatatu aliibua mdahalo kwenye mitandao ya kijamii baada ya kutoa kauli iliyotafsiriwa na wanamitandao  kuwa alikana madai kuwa Samidoh ndiye baba wa mtoto anayetarajia siku za  hivi karibuni.

Karen alikuwa akijibu shabiki mmoja aliyezua madai kwamba Samidoh alikana ujauzito wa mwanasiasa huyo.

Wawili hao wiki jana walirushiana cheche za maneno kila mmoja akionekana kutumia misemo kumkabili mwenzake.

Karen Nyamu kupitia ukurusa wake wa Instagram alikana madai hayo na kuongeza kuwa ujauzito alionao si wa mwanamuziki huyo nguli wa Benga.

“Acheni kujishuku, hajaambiwa mimba ni yake”alisema Karen Nyamu.

Kwa mashabiki ambao wamekuwa wakifuatilia mwanasiasa huyo kwa karibu wameshangazwa na kauli yake kwani yeye ndiye alitangaza kuwa Samidoh alimpa ujauzito Agosti mwaka jana baada ya wawili hao kuzozana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved