logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Karen Nyamu adokeza jinsia na jina la mtoto anayetarajia kujifungua

•Nyamu amedokeza kuhusu jinsia ya mtoto ambaye anatarajia kujifungua hivi karibuni na jina ambalo atakusudia kumpatia.

image
na Radio Jambo

Habari23 February 2022 - 09:58

Muhtasari


•Nyamu amedokeza kuhusu jinsia ya mtoto ambaye anatarajia kujifungua hivi karibuni na jina ambalo atakusudia kumpatia.

Wakili na mwasiasa mashuhuri amedokeza kuhusu jinsia ya mtoto ambaye anatarajia kujifungua hivi karibuni na jina ambalo atakusudia kumpatia.

Katika ukurasa wake wa Instagram, Nyamu amepakia video ya ujauzito wake na kuambatisha na ujumbe unaodokeza kuwa anatarajia mtoto wa kike.

Mama huyo wa watoto wawili ameendelea kudokeza kuwa jina la kitamaduni la mtoto wake litakuwa Njeri.

"Njeri anakuja.. nina raha sana" Nyamu aliandika.

Hata kama Nyamu hajafichua mengi kuhusu mtoto wake, wengi wameuchukua ujumbe wake kama dokezo la mtoto ambaye anatarajia.

Haya yanajri siku chache tu baada ya mgombeaji huyo wa kiti cha useneta wa Nairobi kwa tikiti ya UDA kuzua mdahalo mkubwa kuhusu ujauzito wake.

Karen alichapisha ujumbe ambao uliacha wanamitandao katika hali ya shaka kuhusiana na baba mzazi wa mtoto ambaye amebeba.

“Aache kujishuku, hajaambiwa mimba ni yake” Nyamu alijibu shabiki aliyezua madai kuwa nyota wa Mugithi Samidoh, ambaye anaaminika kuwa baba mzazi wa mtoto huyo alikana ujauzito.

Ujumbe wa Nyamu uliashiria kuwa huenda Samidoh hakuhusika kwenye ujauzito wa tatu wa Nyamu kama inavyotuhumiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved