logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Penzi kikohozi ukificha chozi lasaliti , Zari ashindwa kulificha Gk Choppa ndiye dereva

Zari ameamua kuweka penzi lake wazi baada ya kulificha kwa wiki kadhaa.

image
na

Habari23 February 2022 - 07:47

Muhtasari


•Zari The Boss Lady ameamua kuweka penzi lake wazi baada ya kulificha kwa wiki kadhaa.

•Mpenzi huyo wa zamani wa Diamond Platnumz ameamua kumwaga yaliyomoyoni na kuonyesha  hadharani mpenzi wake mpya kwenye mtandao wa kijamii

Zari na Gk Choppa

Mfanyabiashara na Mwanasosholaiti  mashuhuri Zari Hassani almaarufu Zari The Boss Lady ameamua kuweka penzi lake wazi baada ya kulificha kwa wiki kadhaa.

Mpenzi huyo wa zamani wa Diamond Platnumz ameamua kumwaga yaliyomoyoni na kuonyesha  hadharani mpenzi wake mpya kwenye mtandao wa kijamii.

Pamoja na kukanusha mara si moja kuwa hawana mahusiano na mwanamume huyo, kweli tetesi hizo ziikuwa za kweli .

Si mwajua mapenzi kikohozi hayafichiki, Zari ameamua  kuweka uhusiano wake wazi na  Choppa.

Mama huyo wa watoto watano ameibui gumzo mtaani kwa kile wanamitandao wanasema anatoka kimapenzi na mwanamume aliyemzidi umri huku wengine  wakitabiri kuwa wataachana. 

Kupitia ukurusa wa instagram wa Gk Choppa, amepakia picha wakiwa pamoja na Zari huku wakipigana busu,  kitu ambacho kimewavutia wadaku wa mitandao.

Zari amefikia hatua ya kuonyesha mpenzi wake kwenye mtandao baada ya tetesi kuibuka kwamba Diamond anarusha roho na msanii  Zuchu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved