logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sikuwa najua niliachwa-Carrol Sonnie ajibu madai ya kuachwa kabla ya kujifungua mwanawe

Wawili hao waliachana miezi 2 baada ya kubarikiwa na kifungua mimba wao.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 February 2022 - 10:38

Muhtasari


  • Carrol Sonnie ajibu madai ya kuachwa kabla ya kujifungua mwanawe

Wiki chache zilizopita mcheshi Mulamwah na mama wa mtoto wake Carrol Sonnie wamekuwa wakianikana mitandaoni, na kufichua sababu kuu ya kuachana.

Wawili hao waliachana miezi 2 baada ya kubarikiwa na kifungua mimba wao.

Carrol akiwa kwenye mahojiano na Radiojambo, alikiri kwamba amemsamehe Mulamwah kwa yote ambayo alisema, kwani anamjali mwanawe Keilah.

Huku akijibu madai ya Mulamwah kwamba waliachana akiwa na ujauzito wa miezi 3 Carrol alisema;

"Mimi sikuwa najua kwamba niliachwa nikiwa na ujauzito wa miezi 3, ukweli ni kuwa sikuona, kile najua tuliachana miezi 2 baada ya kubarikiwa na mtoto wangu," Sonnie Alisema.

Aidha Carrol alisema kwamba hakushtuka baada ya Mulamwah kuweka hadharani kwamba wameachana rasmi kwani alikuwa anamjua mpenzi wa Mulamwah.

" Wazazi wake wamekuwa wakinipigia simu na kunishika mkono, sina uhusiano mbaya nao, kwa sasa sitaki kuchumbiana nataka kujijua mwenyewe," Carrol Alizungumza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved