logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zari akiri kumpenda Diamond hata zaidi," Kuliko tulivyokuwa kwenye ndoa"

mwanaume huyo amekuwa hakijaribu kumchumbia kwa Takriban miaka mitatu

image
na

Makala01 March 2022 - 06:12

Muhtasari


•Zari akizingumza kuhusu mahusiano yake mapya na GK Choppa alieleza kuwa amekuwa akijaribu kumchumbia kwa takriban miaka mitatu.

•Alifafanunua kuhusu uhusiano wake na Diamond Platnumz na kudai kuwa hawajawahi kurudiana ila wana ukaribu mkubwa ikizingatiwa kwa kuwa wao ni wazazi wenza.

Zari The Boss Lady

Mwanasoshalaiti mashuhuri Zari Hassan amezuru   Uganda  ambako wanahabari wa nchi hiyo wamepata furasa maalum kumuuliza maswali  yanayohusiana na maisha yake.

Zari akizingumza kuhusu mahusiano yake mapya na GK Choppa alieleza kuwa amekuwa akijaribu kumchumbia kwa takriban miaka mitatu ila  juhudi zake zote zilikuwa zinambulia patupu kwani hakuwahi kumpatia nafasi. Lakini kadiri siku zilivyosonga alibadilisha nia na kuanza kumpenda.

"Sikumpa umakini. Lakini baada ya muda, niliamua kukutana naye na nikagundua kuwa ana moyo mzuri. Ni mtu mzuri,” Zari alisema

Vilevile alifafanunua kuhusu uhusiano wake na Diamond Platnumz na kudai kuwa hawajawahi kurudiana ila wana ukaribu mkubwa ikizingatiwa kwa kuwa wao ni wazazi wenza.

"Naapa, hatujalala pamoja kwa muda mrefu, Sisi ni marafiki tu, kwa sasa  nimekua nikimpenda kuliko hata tulipokuwa wapenzim," Zari alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved