logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wahu awashukuru mashabiki wake kwa kumfanya kuwa maarufu

Nameless kwa kuwa baba wa watoto wake na mume wake

image
na

Habari03 March 2022 - 13:27

Muhtasari


•Msanii maarufu wa kike Wahu amewashukuru mashabiki wake kwa kuendelea kupenda  kazi zake za muziki na kumfanya kuwa maarufu nchini .

wahu 4

Msanii maarufu wa kike Wahu amewashukuru mashabiki wake kwa kuendelea kupenda  kazi zake za muziki na kumfanya kuwa maarufu nchini .

Mama huyo wa watoto wawili anasema wakati fulani alikuwa na huzuni lakini Wakenya bado walimuunga mkono bila kujua shida alizokuwa akipitia kipindi hicho.

Kupitia ukurusa wake wa Instagram, Wahu alieleza kuwa Machi ni mwezi wake wa kuzaliwa na kukiri kuwa hakuwai fikiria kuwa hatawai kuwa mwanamuziki mashuhuri nchini Kenya. 

"Ni mwezi wangu wa kuzaliwa, si unajua mnajua nasikie vizuri nikikutana na watu ambao wananiambia wamekuwa akinisikiza tangu nilipoanza, nakukiri kuwa nimewagusa kwa namna moja au nyingine. Uaminifu  weyu umenifanya kuendelea kufanya zaidi,mimi sikuwai kuwa na mpango wa kuwa maarufu ila nilikuwa nafanya kazi niliyokuwa nikipenda.”

vilevile alimshukuru  Nameless kwa kuwa baba wa watoto wake na mume wake huku akiri kwamba anampenda jinsi alivyo.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved