logo

NOW ON AIR

Listen in Live

King Kaka ahamia Arsenal kufuatia 'uhusiano wa kidhuluma' na Mashetani Wekundu

Ameeleza kutoridhishwa na matokeo hafifu ambayo timu hiyo imekuwa ikiandikisha katika mechi za hivi majuzi.

image
na Radio Jambo

Habari07 March 2022 - 09:51

Muhtasari


•King Kaka ameeleza kutoridhishwa kwake na matokeo hafifu ambayo timu hiyo imekuwa ikiandikisha katika mechi za hivi majuzi.

•Hatua ya King Kaka ilijiri muda mfupi baada ya Mashetani Wekundu kupokea kichapo cha 4-1 kutoka kwa majirani wao Manchester City. 

Mwanamuziki Kennedy Ombima almaarufu King Kaka ametangaza rasmi kuwa kuanzia sasa atakuwa anashabikia timu ya Arsenal.

Kupitia kanda ya video ambayo alipakia Instagram, King Kaka ambaye kwa miaka mingi amekuwa akishabikia Manchester United ameeleza kutoridhishwa kwake na matokeo hafifu ambayo timu hiyo imekuwa ikiandikisha katika mechi za hivi majuzi.

Rapa huyo amesema aliafikia hatua ya kugura United baada ya uhusiano wake na klabu hiyo kuanza kuwa sumu huku akieleza kuwa tayari ameanza kufurahia matunda ya uhusiano wake mpya na 'The Gunners'.

"Kama wengi wenu mnavyojua, nimekuwa katika uhusiano. Uhusiano huo ulianza kuwa sumu, sijakuwa na raha. Nadhani ni wakati murwa nianze kutafuta  raha kwingineko. Nimeanza kupata zawadi kutoka kwa uhusiano wangu mpya. Bidii ambayo uhusiano huo unaweka umefanya nione kuwa kuna  matunda mazuri zaidi. Najitokeza hadharani kutangaza wazi kwamba kwa sasa niko katika uhusiano mpya na najua nitakuwa na raha. Raha sio hakikisho lakini tutafanya ifanye kazi. Ni rasmi kwamba sasa nashabikia Arsenal," King Kaka alisema.

Hatua hii ya King Kaka ilijiri muda mfupi baada ya Mashetani Wekundu kupokea kichapo cha 4-1 kutoka kwa majirani wao Manchester City. Wanabunduki kwa upande wao walipata ushindi wa 3-2 ugenini dhidi ya Watford.

King Kaka amekuwa shabiki sugu wa United kwa muda mrefu ilhali mkewe Nana Owiti amekuwa akiishabikia Arsenal.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved