logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Babalevo asutwa kwa kuvalia chupi yenye nembo feki

Babalevo amesutwa na mashabiki baada ya kuvalia chupi yenye nembo feki.

image
na Radio Jambo

Habari14 March 2022 - 06:35

Muhtasari


• Msanii Babalevo ameshambuliwa na mashabiki kwa kile walichokisema kuwa alikuwa amevalia chupi ghushi.

• “Mpaka sasa sijaona ubaya wowote, nachojua chupi ni chupi tu,” Babalevo aliandika.

 

Instagram, KWA HISANI

Msanii Babalevo ameshambuliwa na mashabiki kwa kile walichokisema kuwa alikuwa amevalia chupi ghushi.

Kupitia picha aliyoipakia kwenye mtandao wa Instagram, Babalevo alionekana kuvalia chupi yenye nembo ya ‘Calvin Kelin’ badala ya nembo halisi ya ‘Calvin Klein.’

Babalevo alichapisha ujumbe kwenye akaunti yake ya Instagram akisema kwamba haoni tatizo lolote kwani chupi ni chupi tu, maadamu inatekeleza wajibu wake wa kufunika uchi.

“Mpaka sasa sijaona ubaya wowote, nachojua chupi ni chupi tu,” Babalevo aliandika.

Baadhi ya wasanii pia kama vile Ommy Dimpoz walichangia mjadala huo huku akiandika kimzaha tu kwamba “…nashangaa watu wana wivu sana, kwani Calvin Kelin amezua?”

Kuna asilimia ya mashabiki waliosimama upande wake huku wengine wakimtaka kuvalia mavazi yenye nembo halisi kwa kuwa  yeye ni msanii mkubwa.

Mara kwa mara watu maarufu wamejikuta katika hali tata na mashabiki wao kutokana na mavazi yao, huku washikadau mbalimbali wakiwataka mashabiki kufahamu kwamba wasanii hao bado ni binadamu  tu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved