logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Dadake Diamond, Esma Platnumz azungumzia suala la mahusiano yake na Zuchu

Esma aliweka wazi kuwa wawili hao, Diamond na Zuchu wapo single kwa sasa

image
na Radio Jambo

Yanayojiri27 March 2022 - 12:37

Muhtasari


•Mama huyo wa wawili  aliidhinisha mahusiano kati ya mastaa hao wawili wa Bongo huku akisema wanafaana.

Diamond na Zuchu

Mfanyibiashara Esma Abdul almaarufu Esma Platnumz ameapa kwamba kamwe hawezi kuingilia mahusiano ya kakake Diamond Platnumz.

Hivi majuzi akihutubia waandishi wa habari katika ukumbi wa Mlimani City, Esma aliweka wazi kwamba hana uhakika wowote  kuhusu mahusiano ya kimapenzi yanayodaiwa kati ya kakake na Zuchu.

"Sina uhakika kwamba ni wapenzi. Ninachokijua mimi ni kuwa ni mtu na bosi wake," Esma alisema.

Mama huyo wa wawili hata hivyo  aliidhinisha mahusiano kati ya mastaa hao wawili wa Bongo huku akisema wanafaana.

Esma aliweka wazi kuwa wawili hao, Diamond na Zuchu wapo single kwa sasa.

"Sio mbaya. Yule ni mwanamke na mwanaume. Mwanaume yuko Single na mwanamke yuko single, sio mbaya," Alisema.

Esma alieleza kuwa familia yake ikiwemo yeye na Mama Dangote inahusika tu katika kuunga mkono kazi za Diamond ila sio kuingilia mahusiano yake. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved