logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zuchu amrukia shabiki aliyedai hajui kuandika jina 'MUNGU'

Zuchu - Mimi ni superstar ndio maana uko hapa unacomment.

image
na Radio Jambo

Habari28 March 2022 - 07:56

Muhtasari


• Na ubaya huo unaoniona nao ninaishi kwenye hekalu nina gari mbili, ya tatu nimeagiza yaja. A superstar ndio maana uko hapa unacomment - Zuchu kwa shabiki aliyemchamba.

malkia wa bongo fleva, Zuchu

Unaambiwa ukiwa maarufu basi mashabiki wako lazima watakuwa wanakufuatilia kwa ukaribu sana tena kwa macho ya umakini kama mwewe katika kila jambo unalolifanya, haswa katika mitandao ya kijamii.

Wikendi iliyopita, msanii Zuchu alipakia kwenye Instagram yake kama kawaida na ambapo aliandika ‘caption’ ambayo shabiki mmoja aliiona kwamba hajaandika jina ‘Mungu’ vizuri.

Shabiki huyo ambaye alishindwa kukaa na hilo dukuduku moyoni aliamua liwe liwalo na kumpasha Zuchu kwa kumsuta kwamba licha ya ukali wote lakini ameshindwa kuandika neno Mungu vizuri eti.

“Neno Mungu limekushinda kuandika ila wewe ulikuwa mbaya hadi nakuzidi,” shabiki huyo kwa jina Shannyog4 aliandika.

Maoni haya ni kama hayakuenda vyema kwa upande wa msanii Zuchu ambaye aliamua kumpasha shabiki huyo na kumnyamazisha ghafla.

“Na ubaya huo unaoniona nao ninaishi kwenye hekalu nina gari mbili, ya tatu nimeagiza yaja. A superstar ndio maana uko hapa unacomment… nasubiri vyako udugu uliyenizidi uzuri,” aliandika Zuchu.

Kwani mtajuaje huyu ni mtoto wa malkia wa mipasho Khadija Kopa, kama hatawapasha mkiingia kwenye kumi na nane zake?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved