logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nipo single!" Mulamwah afichua uhusiano halisi kati yake na kipusa aliyetambulisha kama mpenziwe

Amedai hawajawahi kuwa wapenzi na Val na hawana mpango wa kuchumbiana.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri30 March 2022 - 18:25

Muhtasari


•Mulamwah amesema hakuna  uhusiano wa kimapenzi kati yake na mwanadada ambaye ameaminika kuwa mpenziwe  katika kipindi cha zaidi ya miezi mitatu ambacho kimepita.

•Ruth atakuwa msanii wa pili katika lebo ya mchekeshaji huyo na kibao chake cha kwanza kinatarajiwa kuachiwa Ijumaa.

Mulamwah na Ruth

Mchekeshaji maarufu David Oyando almaarufu Mulamwah amefunguka ukweli kuhusu hali yake halisi ya mahusiano.

Mulamwah amefichua kwamba kwa sasa hachumbiani na yeyote huku akieleza kuwa hakuna  uhusiano wowote wa kimapenzi kati yake na mwanadada ambaye ameaminika kuwa mpenziwe mpya  katika kipindi cha zaidi ya miezi mitatu ambacho kimepita.

Baba huyo wa mtoto mmoja amemtambulisha Ruth kama msanii wake mpya katika lebo yake, 'Mulamwah Ent' na kudai hawajawahi kuwa wapenzi wala hawana mpango wa kuchumbiana.

"Kusema kweli hatujawahi kuchumbiana , na hatuna nia ya kuchumbiana.Haikueleweka. Kwa upande wangu mimi nabaki single na kuzingatia kazi zangu na miradi mingine iliyo mbele yangu," Mulamwah alitangaza kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Ruth atakuwa msanii wa pili katika lebo ya mchekeshaji huyo na kibao chake cha kwanza kinatarajiwa kuachiwa Ijumaa.

Mulamwah alimtambulisha Ruthl kama mpenzi wake mpya takriban miezi mitatu iliyopita , siku moja tu baada ya kutangaza kutengana kwake na Carol Muthoni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved