logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Asiwahi ita jina langu tena,'Hatimaye Eric Omondi amjibu Notiflow

Aliwataka wasanii kuishi kulingana na uwezo wao wala sio kufanya vitu ili kuufurahisha umma

image
na Radio Jambo

Habari01 April 2022 - 12:23

Muhtasari


  • Aliwataka wasanii kuishi kulingana na uwezo wao wala sio kufanya vitu ili kuufurahisha umma na kuwapiga vita wasanii wenzao

Baada ya Notiflow kumshambulia na kumsuta mcheeshaji maarufu nchini Eric Omondi baada ya kumnunulia mpenziwe gari, Eric amejitokea wazi wazi na kumjibu.

Notiflow kupitia ujumbe aliochapisha katika insta story yake, alisema kwamba mastaa wengi wanaiga kitendo chake cha kumzawidi mpenziwe gari ili kuwafurahisha mashabiki ila yote ni uongo.

Aliwataka wasanii kuishi kulingana na uwezo wao wala sio kufanya vitu ili kuufurahisha umma na kuwapiga vita wasanii wenzao ambao wanafanya mambo makubwa.

"Yangu ni mnunulie msichana wangu ggari, kila mtu amekuwa aiaribu kuthibitisha jambo, ati Eric amemnunulia mpenzi wake gari mara kitanda cha mtoto wangi kinagharimu elfu 300,"Notiflow Aliandika.

Kwa upande wake Erick Omondi alimtaka Notiflow kukoma kumtaja kwa kuwa hawapo kwenye viwango sawa.

"Ambieni huyo chokora asiwai ita jina yangu tena," Omondi aliandika.

Notiflow alipakia logbook ya gari alilolinunua katika mtandao wa Instagram, kuonyesha uhalisia wa kitendo chake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved