logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DeSagu adai Spaghetti ilipunguzwa idadi kutoka 210 hadi 191

DeSagu - “Si kawi pekee, walipunguza idadi ya njiti za spaghetti kutoka 210 hadi 191,”

image
na Radio Jambo

Yanayojiri04 April 2022 - 10:11

Muhtasari


• Mchekeshaji Henry DeSagu alilalamika kwamba si tu mafujta ambayo yamepanda bei bali hata watengenezaji wa chakula aina ya Spaghetti walipunguza njiti hizo kutoka 210 hadi 191.

Mchekeshaji Henry DeSagu

Mchekeshaji Henry DeSagu anateta kwamba maisha yanazidi kuwa magumu humu nchini si tu kwa uhaba wa petroli ambao madhara yake yanawakodolea Wakenya wengi macho katika kipindi hiki baki pia katika vyakula.

DeSagu akilalamika kupitia Facebook yake, ameteta kwamba kampuni ya kutengeneza Spaghetti pia ilifanya hujuma kwa wateja wake kwa kupunguza kiwango cha chakula hicho eti.

Kulingana na DeSagu, umakini wake ulimtuma kucvhukua hesabu ya Spaghetti ambazo aligundua kwamba kiwango chake kimepungua kutoka njiti 210 za Spaghetti na eti sasa baada ya kuhesabu alipata zimepungua mpaka njiti 191 kutoka idadi ya awali.

“Si kawi pekee, walipunguza idadi ya njiti za spaghetti kutoka 210 hadi 191,” aliandika DeSagu huku akifuatisha maneno hayo na emoji ya kulia.

Taifa la Kenya linaelekea katika hali mbaya ya kiuchumi baada ya uhaba wa petroli kubisha hodi katika maeneo mengi ambapo shughuli muhimu zimekwama, ikizingatiwa kwamba bidhaa ya petroli hutumika katika kuendesha shughuli viwandani na barabarani.

Haya yanakuja wiki kadhaa tu baada ya baadhi ya wakenya kuanzisha maandamano ya mitandaoni wakitaka bei ya vyakula kupunguzwa almaarufu #Lowerfoodprices.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved