logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fahamu kwa nini mamake Diamond Platnumz anamsukuma afunge ndoa mwezi huu

Mama Dangote aliweka wazi kwamba amemkubali mpenzi mpya wa Diamond

image
na Radio Jambo

Habari05 April 2022 - 09:42

Muhtasari


•Mama Dangote amemtaka mwanawe amvishe pete mpenzi wake baada ya mwezi mtukufu wa wa Ramadhan.

•Mama Dangote aliweka wazi kwamba amemkubali mpenzi wa Diamond na kumshauri atulie sasa na afunge pingu za maisha naye.

Diamond Platnumz na mamake Mama Dangote

Bi Sanura Kassim almaarufu kama Mama Dangote ameendelea kumshinikiza mwanawe, Diamond Platnumz kufanya hara kufunga ndoa na mchumba wake.

Mama Dangote amemtaka mwanawe amvishe pete mpenzi wake baada ya mwezi mtukufu wa wa Ramadhan.

Kulingana na Mama Dangote, Kuna nafasi kubwa la Diamond kupokea baraka zisizo na mwisho kutoka kwa Mwenyezi Mungu katika msimu huu wa sikukuu.

"Mara nyingine tena narudia Nasibu Diamond Platnumz, Mfunge ndoa mwezi huu ukiisha maana baraka zake Allah ndio anazijua," Mama Dangote alimwambia Diamond kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Haya yanajiri baada ya mke huyo wa sasa wa Uncle Shamte kueleza kuridhika kwake na mchumba mpya wa mwanawe ambaye hajatambulishwa.

Mama Dangote aliweka wazi kwamba amemkubali mpenzi mpya wa Diamond na kumshauri atulie sasa na afunge pingu za maisha naye.

"Nashindwa kuelezea furaha yangu mwanangu, Naseeb Diamond Platnumz🦁, hapa sasa umepata mwenza. Utulie babangu uoe," Mama Dangote alisema.

Haya yanajiri huku kukiwa na tetesi kwamba bosi huyo wa WCB alifunga pingu za maisha na mwanadada kutoka Zanzibar katika harusi ya siri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved