logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sisi si marafiki na hatufichi,'Sababu Amber Ray na Phoina sio marafiki tena

Ilithibitishwa Amber alipokosa kujitokeza na kumuunga mkono Phoina

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 April 2022 - 10:05

Muhtasari


  • Wawili hao waliachana  mnamo 2021 na kuwakatisha tamaa wengi waliowaona kama marafiki wa karibu sana

Mwanasosholaiti Amber Ray huku akizindua muziki wake amefichua ni kwa nini yeye si rafiki tena na Phoina.

Wawili hao waliachana  mnamo 2021 na kuwakatisha tamaa wengi waliowaona kama marafiki wa karibu sana.

'Sisi si marafiki na hatufichi. Bado ninaamini katika urafiki kwa sababu bado nina marafiki ambao nimewajua kwa miaka mingi sana.

Maisha yana sababu, na watu pia wana majira katika maisha yetu. Ikiwa inafanya kazi vizuri na nzuri ikiwa hailingani."

Wafanyabiashara warembo walikuwa wakisafiri, karamu, na kusaidia biashara za wenzao. Hata hivyo, mashabiki waligundua kuwa Amber Ray na Phoina hakuonekana kwenye picha za mitandao ya kijamii baada ya Phoina kuzindua duka lake.

Ilithibitishwa Amber alipokosa kujitokeza na kumuunga mkono Phoina alipokuwa akizindua duka lake la kwanza la reja reja jijini Nairobi.

Amber Ray alidokeza kuwa yeye huwa hazungumzii mtu mabaya au kulichafua jina lake haswa ikiwa walileta furaha wakati mmoja maishani mwake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved