logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Ni mtu wetu!" Esma Platnumz azungumzia uhusiano mzuri kati ya kakake Diamond na Harmonize

Esma alimtaja Harmonize kama "mtoto" wa  Diamond na kusema kakake hawezi kubishana naye.

image
na Radio Jambo

Habari14 April 2022 - 04:54

Muhtasari


•Esma alidai kuwa vyombo vya habari na  mashabiki ndio wamekuwa wakitengeneza ugomvi kati ya wasanii hao wawili ilhali kiuhalisia wao wako sawa.

•Mama huyo wa watoto wawili alimtaja Harmonize kama "mtoto" wa  Diamond na kusema kakake hawezi kubishana naye.

Mfanyibiashara Esma Platnumz amefichua kwamba hakuna uhasama wowote kati ya kaka yake Diamond Platnumz na aliyekuwa msanii wake, Harmonize.

Akizungumza na wanahabari katika hoteli ya Hyatt Regency, Esma alidai kuwa vyombo vya habari na  mashabiki ndio wamekuwa wakitengeneza ugomvi kati ya wasanii hao wawili ilhali kiuhalisia wao wako sawa.

"Nyinyi ndio mnawagombanisha. Sio wao. Wao wako sawa kabisa," Esma aliwaambia wanahabari.

Mama huyo wa watoto wawili alimtaja Harmonize kama "mtoto" wa  Diamond na kusema kakake hawezi kubishana naye.

Aliweka wazi kwamba familia ya Wasafi inafurahia mafanikio ya Harmonize kwa kuwa aliwahi kuwa mmoja wao.

"Tunatamani kumuona Harmonize akipiga hatua kwa sababu ni mtu wetu, ametoka kwetu. Tunafurahi akiwa anazidi kupiga hatua. Hamna kinachotuuma kwa kuwa huyo ni mtu wetu. Diamond hawezi kujibizana na mtoto wake," Esma alisema.

Esma alisema kitendo cha Harmonize kumpatia Diamond tuzo lake kiliashiria kuwa bosi huyo wa Wasafi anaheshimika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved