logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rayvanny anunua gari la kifahari kwa Tsh254m

Gari hilo lilimgharimu Rayvanny Tsh 254,000,000. (Ksh13M)

image
na Radio Jambo

Habari15 April 2022 - 04:55

Muhtasari


•Rayvanny alionyesha gari lake jipya kupitia kanda ndogo ya video ambayo alipakia kwenye ukurasa wake wa Instagram.

•Baba Levo alimchana Harmonize kwa kuandika jina la mpenzi wake wa zamani, Kajala Masanja kwenye Range Rover huku akidai kuwa ni kiki tu na gari hilo sio lake.

Staa wa Bongo Raymond Shaban Mwakyusa almaarufu Rayvanny ni mmiliki mpya wa gari la kifahari aina ya V8.

Rayvanny alionyesha gari lake jipya kupitia kanda ndogo ya video ambayo alipakia kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Kulingana na mwanadani wake na mwanamuziki mwenzake Baba Levo, gari hilo lilimgharimu Rayvanny Tsh 254,000,000. (Ksh13M)

"Kitendo cha kuhama kutoka kwenye Prado ya milioni 80 kwenda kwenye Brand New V8 ya milioni 254 unastahili pongezi mdogo wangu Rayvanny," Baba Levo alisema kupitia Instagram.

Wakati huo huo, Baba Levo alimchana Harmonize kwa kuandika jina la mpenzi wake wa zamani, Kajala Masanja kwenye Range Rover huku akidai kuwa ni kiki tu na gari hilo sio lake.

"Wakati Kilandage anatengeneza kiki kwa kuandika magari ya watu majina ya mademu, Rayvanny amenunua Brand New V8 yaani mpyaa," Alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved