logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jux - Kupendeza na kupenda magari mazuri ni kitu nilirithi kutoka kwa baba

Juma Jux - Kupendeza kwangu na kupenda magari mazuri ya kifahari ni kitu nilirithi kutoka kwa babangu mzazi

image
na Radio Jambo

Habari18 April 2022 - 04:35

Muhtasari


• Msanii Juma Jux alisema kwamba mitindo yake ya kifasheni na kupenda magari mazuri ni kitu alichorithi kutoka kwa babake mzazi.

Juma Jux

Mwanamuziki na mjasirimali ambaye pia anajiongeza kama mwanamitindo wa kiume Juma Jux ameweka wazi kwamba kupendeza kwake na mapenzi yake ya dhati kwa fasheni si kitu cha kushtukiza tu maishani mwake bali ni hulka ambayo aliirithi kutoka kwa babake mzazi.

Jux alieleza kwamba hata mtindo wa kutaka kununua na kumiliki magari mazuri ni kitu alichokirithi kutoka kwa mzee wake.

"Mzee wangu alikuwa msafi sana, anajipenda, anaendesha mipira mikali (magari mazuri) nini, kule Lumumba alikuwa anaingiza magari makali anauza.Nakumbuka hata magari yaliyokuwa yanakuja nyumbani kwetu kipindi hicho ni magari makali, yaani ni mzee alikuwa na mipira tu mikali," amesema na kuongeza.

Alisema kwamba alipenda sana kuona baba yake akiingiza magari mazuri aina ya Mercedes Benz na kujisemea kimoyomoyo kwamba ipo siku tu atakuja kuyanunua na pengine kuyamiliki na hilo linampa msukumo fulani wa kuchakarika maishani ili kutimiza azma yake ya kufuata nyayo za mzee wake ambaye sasa ni marehemu.

"Nikasema siku moja nitakuja kuinunua (Mercedes Benz), Baba yangu amefariki muda kidogo, so popote alipo atakuwa anajivunia ninaimiliki sasa"

E-Plus


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved