logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kwisha! Penzi la Rayvanny na Kajala lakata kamba na kuzama

Uvumi uliopo ni kwamba Rayvanny na Paula wameachana na kufuta picha zote za pamoja Instagram.

image
na Radio Jambo

Habari19 April 2022 - 10:45

Muhtasari


• Fununu kutoka Tanzania ni kwamba msanii Rayvanny na mpenzi wake Paula Kajala wameachana.

• Wawili hao wamesitisha kufuatana kwenye mtandao wa YouTube na kufuta picha zote za pamoja.

Fununu zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii ni kwamba penzi kati ya msanii Rayvanny na mpenzi wake Paula kajala limekata Kamba baada ya misukosuko ya muda mrefu.

Inasemekana hatimaye wawili hao wametengana, picha kufutwa na kuacha kufuatana kwenye mtandao wa Instagram ambapo sasa ukitazama vizuri katika orodha ya watu anaowafuata Rayvanny, Paula hayupo pale hali ya kuwa siku za nyuma alikuwa miongoni mmwa watu waliokuwa wakifuatwa na msanii huyo.

Kwa upande wa mwanadada huyo pia ni vivyo hivyo ambapo baada ya kuenda masomoni Uturuki, Rayvanny alikuwa mpweke sana na pengine ndio sababu ya kulitamatisha penzi lao.

Juzi kati Rayvanny aliungana na aliyekuwa mpenzi wake Fahyvanny kusherehekea siku ya kuzaliwa ya mwanawe ambapo wapenzi hao wa zamani walimsherehekea kwa msururu wa picha safi na jumbe maalumu.

Penzi la Rayvanny na Paula ambaye ni mtoto wa muigizaji mkongwe Fridah Kajala liliwekwa wazi baada ya uvumi kuibuka kwamba msanii Harmonize alikuwa akimvizia binti huyo kipindo hicho akiwa bado na mahusiano ya kimapenzi na mamake Fridah Kajala.

Wadau kama vipi hapa Fahyvanny ameamua liwe liwalo penzi la Rayvanny lazima lirudi Tanga, chimbuko la mapenzi lenyewe.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved