logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ndoto yangu ni kuwa kama Diamond Platnumz - Vincent Mboya

Mwanablogu Vincent Mboya amesema kwamba anatamani kuwa na umaarufu kama wa msanii Diamond Platnumz.

image
na Radio Jambo

Habari19 April 2022 - 06:08

Muhtasari


• Vincent Mboya amesema kwamba anatamani kuwa kama Diamond Platnumz.

• Alisema kwamba angependa kuwa na umaarufu mkubwa kadri siku zinavyosonga.



Mwanablogu matata nchini, Vincent Mboya amesema kwamba ndoto yake ni kuwa kama msanii Diamond Platnumz.

Akizungumza katika mahojiano ndani ya Obinna Tv, Mboya alisema kwamba anatamani kuwa na umaarufu mkubwa kama wa Simba, akisema kwamba hali hiyo itamsaidia kubadilisha maisha yake.

Aidha, alikiri kwamba anatamani mazingira ambapo mashabiki watakuwa wakiomba kupiga naye picha kila mahali anapoenda.

"...Yaani mimi natamani sana wakati ambapo kila mahali ninapoenda mashabiki wanaomba kupiga picha na mimi," Mboya alisema.

Mboya alisema kwamba kupitia umaarufu huo anaweza kupata nafasi kadhaa za ubalozi wa kampuni mbalimbali ambapo anaweza kuboresha maisha yake hata zaidi.

Kulingana naye, wasanii na mashabiki wa Tanzania wamefanikiwa kubadilisha kiki zao kuwa manufaa katika gemu la burudani huko Bongo na hivyo kuifanya sekta hiyo kuzidi kufana hata zaidi.

Ifahamike kwamba Wakenya wamekuwa wakimpiga vita Mboya, kwa kile walikisema kuwa anaingilia maisha binafsi ya wasanii. 

Ameshikilia kwamba ataendelea na kazi yake ya kuwakosoa wasanii wakati anapohisi kwamba wanaishi maisha ya uongo na kuwafumba macho mashabiki wao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved