logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera! Njugush na mkewe wanatarajia mtoto wa pili

Wamekuwa katika ndoa kwa takriban miaka sita na tayari wana mtoto mmoja wa kiume pamoja

image
na SAMUEL MAINA

Burudani23 April 2022 - 12:42

Muhtasari


  • •Wanandoa hao walifichua ujauzito katika Tamasha la TTT ambalo waliandaa Ijumaa katika ukumbi wa Nairobi Cinema.

Mchekeshaji Timothy Kimani almaarufu Njugush na mke wake Celestine Ndinda wanatarajia mtoto wao wa pili.

Wanandoa hao walifichua ujauzito katika Tamasha la TTT ambalo waliandaa Ijumaa katika ukumbi wa Nairobi Cinema. Hata hivyo hawakufichua mengi kuhusu safari ya ujauzito huo.

Wawili hao ambao pia ni waigizaji wenza wamekuwa katika ndoa kwa takriban miaka sita na tayari wana mtoto mmoja wa kiume pamoja, Tugi. Walibarikiwa na mtoto wao wa kwanza mwezi Machi, 2018.

Takriban miaka miwili iliyopita, Bi Ndinda alilazimika kujitokeza kuweka mambo wazi kufuatia uvumi uliokuwa umeenea kwamba ni mjamzito.

"Picha hizo ni za ujauzito wangu wa kwanza," Ndinda alijibu kufuatia picha za ujauzito zilizokuwa zinaenezwa.

Njugush na Ndinda walifunga pingu za maisha mwezi Desemba 2016 na wakagundua ujauzito wa mtoto wao wa kwanza rtakriban miezi  minne baadae.

Wawili hao waliwahi kufichua kwamba walikuwa wamekumbwa na uhaba wa fedha katika kipindi ambacho walipata mtoto wa kwanza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved