logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanangu hakukataa kumsalimia Raila Odinga-Jimmy Kibaki azungumza

Walioshiriki walidai mjukuu alikataa kumsalimia kiongozi wa ODM.

image
na Radio Jambo

Habari01 May 2022 - 07:33

Muhtasari


  • Ni video ambayo ilizua mjadala mkali mitandaoni huku, wakenya tofauti wakitoa hisia tofauti kuhusiana na video hiyo

Huku mazishi ya hayati Mwai KIbaki yakiendelea siku ya Jumamosi, viongozi mbalimbali walijitokeza na kuomboleza pamoja na familia ya rais huyo mstaafu.

Kupitia kwenye mitanao ya kijamii video ya kinara wa ODM Raila Odinga akimsalimia mjukuu wa Mwai na kisha akakataa ilienea.

Ni video ambayo ilizua mjadala mkali mitandaoni huku, wakenya tofauti wakitoa hisia tofauti kuhusiana na video hiyo.

Walioshiriki walidai mjukuu alikataa kumsalimia kiongozi wa ODM.

Fact-checker hata hivyo imethibitisha kuwa video imehaririwa kwa nia ambayo bado haijajulikana.

Mdadisi huyo amegundua kuwa mjukuu huyo alimsalimia waziri mkuu huyo wa zamani na ni baada ya kumsalimia ndipo alipompa mgongo.

Huku Jimmy KIbaki akizungumzia suala hilo, kupitia kwenye ukurasa wake rasmia ya twitter amesema kwamba mwanawe hakukataa kumsalimia kinara huyo.

Zaidi ya yote amewauliza wakenya kuelewa kuhusu hisia za mtu,na kwamba familia yao inapitia wakati mgumu.

"Hakuna anayeweza kudhibiti hisia. Mwanangu hakukataa kumkumbatia Rt mheshimiwa Raila Odinga. Sisi kama familia tunakabiliwa na nyakati ngumu. Kuelewa hisia," JImmy Alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved