logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nadia Mukami afunguka kuhusu suala la kubadili dini

Arrow Bwoy ni mfuasi wa dini la Kiislamu ilhali Nadia ni Mkristo.

image
na Radio Jambo

Makala09 May 2022 - 10:52

Muhtasari


•Mwanamuziki huyo amefichua kuwa mumewe hajawahi kumpatia shinikizo lolote la kubadilisha dini yake.

•Ameweka wazi kuwa huwa wanaelewana vizuri na kufurahia penzi lao licha ya tofauti za kidini zilizopo kati yao.

Mwanamuziki Nadia Mukami ameweka wazi kuwa tofauti ya dini kati yake na Arrow Bwoy sio tatizo kwenye mahusiano yao.

Nadia amefichua kuwa mumewe hajawahi kumpatia shinikizo lolote la kubadilisha dini yake. Arrow Bwoy ni mfuasi wa dini la Kiislamu ilhali Nadia ni Mkristo.

 "Hajawahi kunipa pressure. Dini ni suala nyeti sana kwangu. Kuna vitu ambavyo sipendi kuzungumzia; serikali, dini, kikundi cha wachache ni mambo ambayo sipendi kuzungumzia kwa kuwa naweza kusema kitu kiumize mtu fulani na mashabiki ni aina tofauti," Nadia alisema akiwa kwenye mahojiano na Eve Mungai.

Malkia huyo wa muziki mwenye umri wa miaka 25 amesema kuwa kwa sasa upendo ndio dini yake na kipenzi chake.

Nadia ameweka wazi kuwa huwa wanaelewana vizuri na kufurahia penzi lao licha ya tofauti za kidini zilizopo kati yao.

"Huwa tunaombeana.Tuna furaha. Huwa tunaelewana. Kama vile wanandoa wengine huwa tunakosana kidogo. Kitu ninachopenda kutuhusu ni kuwa  tunaelewana  sana. Sisi ni marafiki, yeye ni bestie yangu. Tunafurahia hadi tukunje mgongo," Alisema Nadia.

Katika jamii ya Waafrika, ni kawaida kwa wanawake kubadilisha dini yao pindi wanapoolewa na mwanaume wa dini tofauti.

Mwanamuziki Tanasha Donna alipojitosa kwenye mahusiano na Diamond Platnumz alijiunga na dini ya staa huyo wa Bongo ya Kiislamu.

Wengi wamekuwa wakisubiri kuona ikiwa Nadia atapiga hatua kama hiyo baada ya mahusiano yake na Arrow Bwoy kuwa wazi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved