Mimi nitajiri sitawahi kuwa broke maishani-Eric Omondi awajibu wanaodai hana pesa

Muhtasari
  • Mcheshi maarufu nchini Eric Omondi amejitokeza wazi kuzungumzia madai kwamba ana mikopo hana pesa za kujikimu
Image: INSTAGRAM// ERIC OMONDI

Mcheshi maarufu nchini Eric Omondi amejitokeza wazi kuzungumzia madai kwamba ana mikopo hana pesa za kujikimu.

Hii ilikuwa baada ya Melina kudai kuwa Eric Omondi alikosa kumlipa ksh. 450,000 anazodaiwa.

Akiongea kwenye mahojiano na, Eric Omondi alisema kuwa ana mamilioni ya pesa na bado anaingiza mamilioni ya pesa, ana show 3 nje ya nchi mwezi huu na hii itamfanya apate mamilioni ya pesa.

Eric alisema kuwa safari yake katika uwanja wa burudani imekuwa ya mafanikio na amepata pesa nyingi na ana uhakika sana kwamba katika maisha yake yote ambayo hatawahi kuwa broke.

Eric alisema kuwa Mungu amembariki na wanaomuombea akue broke hawataweza kutokea.

Haya yanajiri siku chache baada ya msanii wa injili mwenye utata Ringtone, kusema kwamba Eric hana pesa na amekopa kila mahali ili aweze kujikimu.

Ringtone Apoko pia badala yake  alisema anamfahamu Eric Omondi zaidi na hata marafiki zake.

Eric Omondi amekuwa akitoa wito kwa vyombo vya habari kucheza muziki wa Kenya, huku akifanya kazi nyuma ya pazia na Harmonize ili kukuza muziki wa Tanzania.