logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wafahamu wasanii wa Afrika wanaomiliki ndege za kibinafsi

Diamond alitangaza mpango wake siku wa Jumatano.

image
na Radio Jambo

Habari12 May 2022 - 10:55

Muhtasari


•Diamond alitangaza mpango wake siku wa Jumatano wakati alipokuwa anamtakia meneja wake El-Jefe Mendez heri za siku ya kuzaliwa.

•Familia ya Cuppy inaripotiwa kumiliki ndege ya kibanfsi ambayo msanii huyo hutumia katika ziara zake.

Diamond Platnumz, DJ Cuppy, Davido

Ni rasmi kwamba nyota wa Bongo Diamond Platnumz anatazamia kununua ndege kufikia mwisho wa mwaka huu. 

Diamond alitangaza mpango wake siku wa Jumatano wakati alipokuwa anamtakia meneja wake El-Jefe Mendez heri za siku ya kuzaliwa.

"Tulinunua 2021 Rolls Royce Black Bedge Zero Kilometre mwaka jana, na tunanunua ndege ya kibinafsi mwaka huu!! hiyo ndio tafsiri ya kuwa na usimamizi bora!! Ni Siku ya Kuzaliwa ya meneja wangu Sallam Sk," Diamond aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Bosi huyo wa WCB hata hivyo hatakuwa msanii wa kwanza barani Afrika kumiliki ndege ya kibinafsi.

Kuna baadhi ya wasanii na watu mashuhuri hasa kutoka Afrika Magharibi ambao wamewahi kununua ndege za usafiri wao wa kibinafsi.

1. Davido

Mwanamuziki wa Afropop David Adedeji Adeleke almaarufu Davido anaripotiwa kumiliki ndege aina ya Bombardier Global Express 6000.

Raia huyo wa Nigeria alinunua ndege hiyo inayodaiwa kugharimu mabilioni ya pesa miaka michache iliyopita.

2. Wizkid

Wizkid ni msanii mwingine wa Afropop kutoka Nigeria anayeripotiwa kuwa mmiliki wa ndege ya kibinafsi.

3. DJ Cuppy

Mchezasanturi wa Florence Ifeoluwa Otedola almaarufu DJ Cuppy ni msanii ambaye amebahatika kuzaliwa katika familia ya kitajiri.

Familia ya Cuppy inaripotiwa kumiliki ndege ya kibanfsi ambayo msanii huyo hutumia katika ziara zake.

4. Don Jazzy

Mzalishaji mashuhuri Don Jazzy pia anaaminika kuwa miongoni mwa wasanii wa Nigeria wanaomiliki ndege za kibinafsi.

Jazzy anapendelea kufanya ziara zake za kimataifa kutumia ndege ya kibinafsi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved