logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Juma Jux:Mimi sio mchumba wa Huddah Monroe ni rafiki tu

Hakuna kitu kama hicho. Haipo. hiyo ya? Ilikuwa zamani huko hii haihusiki na hapa '

image
na Radio Jambo

Yanayojiri16 May 2022 - 12:32

Muhtasari


  • Akihojiwa Jumapili ya Mei 15, Jux alisema ni marafiki wanaojumuika sana
Juma Jux

Mwimbaji wa bongo fleva Juma Jux amezungumzia tetesi kuwa anachumbiana na mwanasosholaiti wa Kenya Huddah Monroe.

Akihojiwa Jumapili ya Mei 15, Jux alisema ni marafiki wanaojumuika sana.

Lakini alipingwa kuhusu uhusiano wao wakati video ya wawili hao yenye kudokeza ilipoibuka mtandaoni. Alicheka na kutikisa kichwa kukataa.

Hakuna kitu kama hicho. Haipo. hiyo ya? Ilikuwa zamani huko hii haihusiki na hapa '

Siku chache zilizopita, Huddah Monroe alikuwa Afrika Kusini na Juma Jux. Kulikuwa na ushahidi wa video kuonyesha walikuwa pamoja.

Lakini katika mahojiano haya ya hivi karibuni, Jux alisema hiyo haimaanishi kuwa wanachumbiana au ni wappenzi.

Walipigwa picha pamoja na wakati mmoja, Monroe pia alionekana akiwa amevaa koti lake alilolipenda zaidi.

Jux sasa anasema kuwa lebo yake ni maarufu sana na labda aliinunua ili kukuza brand yake.

"Mimi nipo kwenye mahusiano na najua Huddah yuko kwenye uhusiano wa kimapenzi. Kwahiyo swala la sisi wawili kuwa wapenzi halijitokezi. Lakini nitalijibu swali hili siku nyingine. Lolote linaweza kutokea."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved