logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nilikuwa naruka karibu nianguke mtoto akilia,'Mwigizaji Selina asimulia jinsi kumlea mwanawe kumembadilisha

Mwigizaji huyo alibarikiwa na kifungua mimba wake wiki 3 zilizopita

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 May 2022 - 09:42

Muhtasari


  • Ndio katika kumlea mtoto kuna changamoto zake haswa kama wewe ni mama kwa wakati wa kwanza
Celestine "Selina" Gachuhi

Celestine Gachui alifahamika sana mitandaoni baada ya kuigiza katika kipindi cha Selina kilichokuwa kinapeperushwa kwenye runinga ya Maisha Magic East.

Mwigizaji huyo alibarikiwa na kifungua mimba wake wiki 3 zilizopita, ambaye kupitia kwenye chaneli yake ya Youtube amesimulia jinsi mwanawe amebadilisha maisha yake na jinsi amekabiliana na changamoto kama mama.

Ndio katika kumlea mtoto kuna changamoto zake haswa kama wewe ni mama kwa wakati wa kwanza.

"NIlikataa hospitali kwa siku chache,sikuwa najua kwamba mtoto alifaa kudungwa sindano, sikuelewa kwa nini lakini nilihisi kama moyo wangu ungetoka, baada ya kuruhusiwa na kuenda nyumbani nilishindwa nini nini kitatendeka, usiku singelala vyema," Alisimulia Selina.

Aliongeza;

"Nikiwa hospitali sikuwa naweza kutoa maziwa kwa hivyo nilikunywa dawa, baada ya kuenda nyumbani mtoto wangu alikataa kunyonya, sikuwwa nalala, nilikuwa naamka nikiwa nimeshtuka mtoto akilia,akipiga kelel nilikuwa naruka karibu nianguke

Nilikuwa nalala na taa kwa sababu nilikuwa na mshangao sana kwamba kitu kinaweza kutokea. Hospitalini, niliamka na hakuna taa mtoto alikuwa analia na nilishtuka sana. Nilitokwa na jasho kila mtoto alipokuwa akilia.”

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved