logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilipunguza ulevi baada ya kupata ujauzito wa kwanza- Avril

Avril hata hivyo ameweka wazi kuwa yeye si mnywaji wa Pombe mara kwa mara.

image
na Radio Jambo

Habari19 May 2022 - 09:28

Muhtasari


•Avril amesema alipunguza tabia yake ya kunywa pombe baada ya kupata ujauzito wa mtoto wake wa pekee.

•Katika kipindi hicho Avril pia alipongeza uteuzi wa Martha Karua kuwa mgombea mwenza wa , Raila Odinga.

Mwanamuziki mashuhuri Judith Nyambura almaarufu Avril amekiri kuwa mtumizi wa kileo aina ya Vodka.

Avril hata hivyo ameweka wazi kuwa yeye si mnywaji wa Pombe mara kwa mara. Amesema alipunguza tabia yake ya kunywa pombe baada ya kupata ujauzito wa mtoto wake wa pekee.

"Mimi hupendelea Vodka. Hapo awali nilikuwa nakunywa Whisky lakini imekuwa kali kiasi kwangu sasa kwa sababu sijakuwa nikilewa sana hasa baada ya ujauzito wangu. Sikunywa pombe yoyote katika kipindi hicho. Kwa sasa sikunywi pombe sana," Avril alisema katika kipindi cha maswali na majibu kwenye Citizen Digital.

Mama huyo wa mtoto mmoja pia alisema anafurahia hatua yake kuwa mzazi hasa kila  anapomtazama mwanawe akikua.

"Ninajiona sana ndani yake. Kila siku huwa siku tofauti. Huwa anajifunza kitu kipya," Alisema.

Avril alifichua kuwa anakusudia kupata angalau mtoto mmoja ana wawili zaidi. Hata hivyo alisema hayupo tayari kupata mtoto mwingine hivi karibuni.

"Mtoto mwenye niko naye kwa sasa ananikimbiza. Gharama ya kulea mtoto ni kubwa kila mahali. Ningependa kupata wengine wawili ama watatu. Kifungua mimba wangu anaweza kupata ndugu wengine. Kwa sasa naamini biashara yangu ndiyo mtoto wa pili," Alisema.

Katika kipindi hicho Avril pia alipongeza uteuzi wa Martha Karua kuwa mgombea mwenza wa mpeperusha bendera ya Azimio la Umoja, Raila Odinga.

Alisema anafurahia uteuzi huo kwa kuwa ni wakati muhimu kwa nchi ya Kenya huku akimtakia mafanikio azma yake ya siasa.

"Kuweza kujiinua jinsi alivyojiinua ni jambo la kufurahisha. Niko na picha naye. Namtakia kila la kheri. Ni wakati muhimu katika historia," Alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved