logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwigizaji Omosh azungumza baada ya kuombewa na Pastor Kanyari

Omosh alisema yupo tayari kutengeneza madhabahu yake na Mungu vizuri

image
na Radio Jambo

Burudani23 May 2022 - 13:32

Muhtasari


  • Mwigizaji Omosh azungumza baada ya kuombewa na Pastor Kanyari

Mwigizaji Joseph Kinuthia almaarufu Omosh amekuwa gumzo tena mitandaoni baada ya video yake akianguka wakati akiombewa na mhubiri mashuhuri Victor Kanyari kusambaa.

Katika video hiyo Omosh anaanza kwa kujitambulisha kisha anaendelea kueleza jinsi alivyojipata katika kanisa la Kanyari.

Mwigizaji huyo wa Tahidi High alieleza kuwa aliamua kupiga hatua hiyo baada ya rafiki yake kumshawishi ahudhurie ibada ya kanisa. Baada ya ibada ndipo Kanyari alimpatia msanii huyo nafasi ya kutoa ushuhuda wake.

"Leo nimesoma kuhusu madhabahu. Nikiwa nimekaa pale chini nimeona labda mambo yangu huenda mrama kwa kuwa sijajenga madhabahu vizuri. Hapa nimesoma lazima nijenge madhabahu yangu ili naye Mungu ashuke anene nami," Omosh alisema mbele ya waumini waliokuwa wamejumuika pale kanisani.

Omosh alisema yupo tayari kutengeneza madhabahu yake na Mungu vizuri baada ya kusikiliza mahuburi ya Kanyari.

Huku akizungumzia video hiyo ambayo imeenea sana mitandaoni alisema kuwa;

"I'm on a rooftop, I'm high and I am with the most high and I have the spirit, but not Konyagi. Try God so you can feel the high I feel. Ah maisha  joh tukicheki mazee niko rooftop niko place high yani na niko place high na niko na the most high na niko na spirit na sio ya konyagi, try him, try God usikie vile nasikia niko high na most high au sio?"

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved