logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nilipitia mengi" Msanii Jovial afunguka kuhusu kukumbwa na msongo wa mawazo

Jovial ameeleza kuwa alipitia mwishoni mwa mwaka jana na mwanzoni mwa mwaka huu.

image
na Radio Jambo

Habari27 May 2022 - 08:38

Muhtasari


•Jovial amefichua kuwa alikumbwa na msongo wa mawazo mwishoni mwa mwaka jana na mwanzoni mwa mwaka huu.

•Amewashauri watu kushirikisha wapenzi wao kwenye mambo wanayokumbana nayo maishani ili kutafuta suluhu ya haraka.

Malkia wa muziki Juliet Miriam almaarufu Jovial amefichua kuwa alikumbwa na msongo wa mawazo miezi michache iliyopita.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Jovial ameeleza kuwa alipitia mwishoni mwa mwaka jana na mwanzoni mwa mwaka huu.

Jovial hata hivo amebainisha kuwa sio watu wengi walifahamu kuhusu yale ambayo alikuwa anapitia kwa kuwa alificha hisia zake halisi kutoka kwa mitandao ya kijamii.

Nilikuwa na huzuni, kuharibika na kupoteza kabisa lakini hakuna mtu alijua kuhusu hilo! Kwenye mitandao ya kijamii kila mtu anafuraha, ndivyo tunavyotakiwa kuonyesha lakini ndani yetu tunakufa polepole," Jovial aliandika kwenye Instastori zake.

Mwanamuziki huyo kutoka Pwani ametumia hali yake kufahamisha watu kuhusu msongo wa mawazo.

Amewapa matumaini watu ambao wanakabiliwa na hali kama hiyo kwa sasa na kuwahakikishia kuwa kila hali huja kupita kadri siku zinavyosonga.

"Hata upitie changamoto ya aina gani itapita tu! Natumai nitaweza kusaidia mtu mahali. Shikilia hapo kesho ni siku mpya mpenzi na mwangaza," Alisema.

Jovial amefichua kuwa huwa anapenda kufunga kuhusu mambo anayokumbana nayo ili aweze ili aweze kukutana na watu wanaopitia hali zinazofanana.

Amewashauri watu kushirikisha wapenzi wao kwenye mambo wanayokumbana nayo maishani ili kutafuta suluhu ya haraka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved