logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nakiri nilimkosea Diamond Platnumz,'Rafikiye Harmonize amuomba Diamond msamaha

Hbaba amegundua makosa yake na amejishusha na kuomba msamaha

image
na Radio Jambo

Habari30 May 2022 - 11:44

Muhtasari


  • Rafikiye Harmonize amuomba Diamond msamaha

Rafiki mkubwa wa Harmonize na mmoja wa watu ambao wamekuwa wakishirikiana na Harmonize kumchana Diamond Platinumz mtandaoni Hbaba hatimaye amejitokeza wazi na kumuomba Diamond Platinumz amsamehe kwa mabaya yote na mambo aliyomfanyia.

Hbaba walikuwa miongoni mwa marafiki wa karibu wa Harmonize ambao walikuwa wakisema ni kweli Diamond Platinumz anatumia nguvu za giza, alienda hadi kushambulia maisha ya kibinafsi ya Diamond na kudai kuwa hana uwezo wa kununua Rolls Royce asilia.

Baada ya kuachana na Harmonize, Hbaba amegundua makosa yake na amejishusha na kuomba msamaha kwa Diamond Platinumz na wafanyakazi wote wa Wasafi.

"Binadamu tujifunze kuomba msamaha kwa mtu uliemkosea, Nakili mbele yenu nilimkosea saaana @diamondplatnumz Narudia Nisamehe @diamondplatnumz, Ukweli nimeujua wee ni mtu wa watu kweli kweli @diamondplatnumz Unaroho yakipekee saaana sijawai ona kwakweli wee ni PEPONI moja kwa moja, kumsamehee @h.baba_ PEPONI moja kwa moja @sallam_sk @babutale @mkubwafellatmk (PEPONI MOJA KWA MOJA) MASHABIKI WA WASAFI MNISAMEHE... WASAFI CHAMA LANGU," Alliandika Hbaba.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved