logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilikuwa nimeolewa kwa miaka 4-Huddah Monroe afichua siri yake kubwa

Mjasirimali huyo anafahamika sana mitandaoni kwa ajili ya biashara yake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri09 June 2022 - 20:54

Muhtasari


  • Huddah alifichua kuwa alikuwa ameolewa kwa muda si mmoja bali miaka minne akiwa na umri mdogo wa miaka 19 na mwanamume ambaye hakufichua jina lake
Mwanasosholaiti Huddah Monroe

Huddah Monroe aliamua kufichua na kufunguka kuhusu maisha yake kupitia ukurasa wake wa instagram huku akiwafahamisha mashabiki mambo ambayo hawakuwa wanayajua kumhusu.

Mjasirimali huyo anafahamika sana mitandaoni kwa ajili ya biashara yake.

Mjasiriamali aliyefanikiwa alichukua hadithi zake za insta kushiriki kile alichotaja kuwa siri yake kuu.

Huddah alifichua kuwa alikuwa ameolewa kwa muda si mmoja bali miaka minne akiwa na umri mdogo wa miaka 19 na mwanamume ambaye hakufichua jina lake.

Haikuwa hivyo tu,  aliongeza kuwa wawili hao hawakupata watoto kwa sababu mwanamume wake alikuwa mraibu wa dawa za kulevya.

"Nilikuwa kwenye ndoa kwa miaka 4 @ 19, hatukuwa na mtoto na tukaachana kwa  sababu mwanaume alikuwa mlevi wa dawa za kulevya! Sikuwa maarufu kwa hivyo sikuhitaji kuitangaza! So naongea kwa uzoefu. Si mzaha nyinyi nyote! Usiku mwema! Hiyo ndiyo siri yangu kubwa." Soma chapisho la Huddah.

Ufichuzi wa Huddah unajiri siku chache baada ya kukiri kuchumbiana na mwanamume Mtanzania akisema wawili hao walikuwa wakipanga kufunga ndoa hivi karibuni.

Mrembo huyo alikuwa akizungumza kwenye mahojiano na vyombo vya habari vya Tanzania lakini alikataa kutaja mtu huyo wa ajabu ni nani.

"Hivi karibuni,namchumbia  mtu nchini Tanzania," alisema.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved