logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sitawahi piga kura-Huddah Monroe akiri

Mwanasosholaiti huyo kwenye Instagram yake alisema hatapiga kura katika uchaguzi Mkuu ujao

image
na Radio Jambo

Yanayojiri14 June 2022 - 09:17

Muhtasari


  • Pia aliwahimiza wananchi kuwa na amani wakati wa uchaguzi na kuepuka kujihusisha na vurugu
Instagram, KWA HISANI

Mwanasosholaiti maarufu nchini Huddah Monroe kupitia ukurasa wake wa instagram amewashangaza wengi baada ya kufichua kwamba hajawahi piga kura.

Mwanasosholaiti huyo kwenye Instagram yake alisema hatapiga kura katika uchaguzi Mkuu ujao utakaopangwa kufanyika Agosti mwaka huu.

Kulingana na Huddah, yeye ni mlipa kodi tu anayeishi maisha yake na kutazama pembeni. Hata hivyo, alisema kuwa anatetea watu kupiga kura.

"Sijawahi kumiliki kadi ya wapiga kura. Sijawahi kupiga kura. Ninatetea upigaji kura lakini sitawahi kupiga kura. Sarakasi sio yangu. Ni mlipakodi anayeishi maisha yake akitazama pembeni. Na kutajirisha familia za viongozi wenu. ili waendelee kuishi kwa wingi."

Pia aliwahimiza wananchi kuwa na amani wakati wa uchaguzi na kuepuka kujihusisha na vurugu.

"Sijali nani atakaye shinda ajenda zao haziwahi saidia familia yangu wala kunisaidia ndio maana inaniuma nikiona watu wakipigana kwa ajili ya watu ambao hawawajali na wala kusaidia familia yao, tuweni na amani."

Aidha amewahimiza wanasiasa wasilete vurugu endapo watashindwa kwenye uchaguzi mkuu.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved