logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nitaacha urithi bora bila watoto!' Mjukuu wa Kibaki afichua sababu hataki watoto

Andrew alisema angependelea kuitwa mjomba badala ya kuwa na watoto wake mwenyewe.

image
na Radio Jambo

Burudani21 June 2022 - 10:59

Muhtasari


•Mwanamitindo huyo alibainisha kuwa angependelea kuitwa mjomba badala ya kuwa na watoto wake mwenyewe.

•Aliweka wazi kuwa kwa sasa hayupo kwenye mahusiano yote na hayupo makini kutafuta mpenzi.

Mjukuu wa rais wa tatu wa Kenya Mwai Kibaki, Sean Andrew amesisitiza kuwa hataki kuwahi kupata watoto.

Mwaka jana Andrew aliwashangaza wengi baada ya kudai kuwa hajawahi kupatwa na wazo la kuwa baba.

“Ndio nimewahi fikiria kuoa na kutulia katika ndoa lakini hata siku moja sijawahi jifikiria au kujiona kuwa baba. Pengine niwe mume tu lakini sitaki watoto,” Alisema katika kipindi cha Q&A kwenye Instagram.

Katika mahojiano ya hivi majuzi, Andrew aliweka wazi kuwa ni angepelea kuwafuga wanyama kipenzi wanyama kuliko watoto.

Aidha, mwanamitindo huyo alibainisha kuwa angependelea kuitwa mjomba badala ya kuwa na watoto wake mwenyewe.

"Sijui, ni wazo ambalo lilinikujia kwa muda mrefu. Watoto hawajakuwa mojawapo ya ajenda zangu. Nadhani nitaacha urithi bora bila watoto," Andrew alisema katika mahojiano na Mpasho.

Ingawa hataki kupata wake mwenyewe, Andrew aliweka wazi kuwa hana chuki yoyote dhidi ya watoto.

"Watoto ni wazuri lakini sijawahi kujiona kama baba," Alisema.

Mtoto huyo wa mfanyibiashara Jimi Kibaki hata hivyo hakutupilia mbali suala la kuwahi kujitosa kwenye ndoa.

"Ikitokea ningependa kuwa kwenye ndoa, ningependa kushiriki maisha yangu na mtu. Lakini sitazamii hilo," Alisema.

Andrew alifichua kuwa hapo awali amewahi kuwa kwenye mahusiano kadhaa lakini hakuna ambayo yalifua dafu.

Aliweka wazi kuwa kwa sasa hayupo kwenye mahusiano yote na hayupo makini kutafuta mpenzi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved