logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Siamini kama Kajala ni wangu-Harmonize

Msanii huyo alimshukuru Mungu kwa kumpa nafasi nyingine ya kuwa na mpenzi wake

image
na Radio Jambo

Burudani05 July 2022 - 14:43

Muhtasari


  • Siku chache baaada ya kumvisha mpenzi wa maisha yake pete msanii wa bongo Harmonize akiwa kwenye mahojiano amesema kwamba bado hajaamini kwamba Kajala ni wake
Harmonize na Kajala

Siku chache baaada ya kumvisha mpenzi wa maisha yake pete msanii wa bongo Harmonize akiwa kwenye mahojiano amesema kwamba bado hajaamini kwamba Kajala ni wake.

Kabla ya kumvisha pete Harmonize alivuma mitandaoni kwa kumuomba Kajala msamaha hadharani na hata kumnunulia zawadi za bei ghali ili aweze kumsamehe.

"Kuna wakati mtu huamini kabisa kinachotokea kwenye maisha yako, mimi siamini kabisa kama K (Kajala) ni wangu sasa,"Alizungumza Harmonize.

Msanii huyo alimshukuru Mungu kwa kumpa nafasi nyingine ya kuwa na mpenzi wake, huku akiai kwama kuwa au kuoa mtu ambaye anakupa raha ni zawadi ya kipekee duniani.

“Mwenyezi Mungu ni mwema sana, amenisogeza karibu kabisa na mwanamke wa maisha yangu, maana nitampenda siku zote, nampenda mno furaha ya maisha yangu ipo mikononi mwake sasa."

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved