logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Tunapaswa kujaza dunia!" Diamond ajibu madai ya kuwa na watoto kote Afrika

"Tunapaswa kujaza dunia. Tulitumwa kufanya hivo!" Diamond alisema

image
na Radio Jambo

Makala18 July 2022 - 10:01

Muhtasari


•Diamond aliweka wazi kuwa amewahi kupata watoto na wanawake pekee ambao alichumbiana nao kwa muda.

•Diamond alisisitiza kwamba ni wajibu wa mwanadamu kuijaza dunia kama alivyoagizwa na Mungu.

Staa wa Bongo Naseeb Abdul Juma almaarufu Diamond Platnumz amepuuzilia mbali madai kuwa ana watoto kote Afrika.

Akiwa kwenye mahojiano na DW Afrika, Diamond aliweka wazi kuwa amewahi kupata watoto na wanawake pekee ambao alichumbiana nao kwa muda.

"Sijawahi kupata mtoto na mtu ambaye sikutaka kupata naye ama kimakosa. Ata kama ilifanyika lazima iwe mtu ambaye tulikaa naye kwa muda, sio kimakosa," Diamond alisema.

Bosi huyo wa WCB aliweka wazi kuwa hakuna watoto wake wasiojulikana hadharani ambao alipata na wanawake wengine huko nje.

Pia alibainisha kuwa kwa kawaida huwa anaonyesha watoto wake wote kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii.

"Ukienda kwenye ukurasa wangu utaona huwa napakia watoto wangu pale," Alisema bila kusita.

Diamond alisisitiza kwamba ni wajibu wa mwanadamu kuijaza dunia kama alivyoagizwa na Mungu. Hata hivyo alidinda kuthibitisha idadi halisi ya watoto wake.

"Tunapaswa kujaza dunia. Tulitumwa kufanya hivo. Ni kwamba tunapaswa kuifanya vyema na kwa njjia ipasavyo. Lakini tulitumwa kuhakikisha tumejaza dunia," Alisema.

Licha ya mashaka mengi kuhusu idadi ya watoto wake, Diamond ana watoto wanne pekee wanaojulikana hadharani.

Latifah Dangote na Prince Nillan ni watoto wake wa kwanza ambao alipata na mwanasoshalaiti maarufu Zari Hassan.

Mwaka wa 2017, staa huyo alipata mtoto wa kiume na mwanamuziki Hamisa Mobetto katika kipindi kifupi cha mahusiano yao.

Baadae Diamond alijitosa kwenye mahusiano na msanii wa Kenya Tanasha na wakabarikiwa na mtoto wa kiume, Naseeb Junior, mwakani 2019.

Mara nyingi bosi huyo wa Wasafi ameshtumiwa kwa kuwapendelea zaidi watoto wake wawili wa kwanza ambao alipata na Zari.

Kwenye kurasa zake, Diamond amekuwa akiwapakia Tiffah Dangote na Prince Nillan zaidi ya wanawe wengine wawili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved