logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mungu ametenda-Ujumbe wa mkewe Rais mteule Rachel Ruto kwa mumewe

Aliendelea kunukuu andiko kutoka katika Biblia; Waebrania 10:23 inayosema,

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 September 2022 - 12:26

Muhtasari


  • Mke wa rais mteule Mama Rachel Ruto ameandika ujumbe mzito kwa mumewe William Ruto ambaye uchaguzi wake uliidhinishwa na Mahakama ya upeo

Mke wa rais mteule Mama Rachel Ruto ameandika ujumbe mzito kwa mumewe William Ruto ambaye uchaguzi wake uliidhinishwa na Mahakama ya upeo.

Rachel alipongeza ushindi wa hivi punde wa Ruto muda mfupi baada ya Mahakama ya upeo kutoa uamuzi wake.

“Hongera Bill mpenzi wangu. Mungu amefanya. Ninajivunia wewe! Akupe neema na hekima ya kuiongoza Kenya katika ukuu! Ulizaliwa na ulikusudiwa kwa hili!” alisema.

Aliendelea kunukuu andiko kutoka katika Biblia; Waebrania 10:23 inayosema,

"Na tushike kwa nguvu bila kuyumbayumba kwa tumaini tunalothibitisha kwamba Mungu anaweza kuaminiwa kutimiza ahadi yake."

Mke wa rais anayekuja pia aliongoza maombi katika makazi ya Naibu Rais huko Karen, ambapo watakuwa wakihama katika wiki zijazo.

Mahakama ya upeo imetangaza kwamba matokeo ya uchaguzi wa urais wa 2022 yaliyotangazwa na Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati yameidhinishwa.

Chebukati alikuwa amemtangaza Ruto kuwa rais mteule baada ya kupata kura 7,176,141 (50.49%) dhidi ya kura 6,942,930 (48.85%) za mgombea urais wa Azimio la Umoja Raila Odinga.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved