logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto Mlinde Mama wa taifa dhidi ya Wachungaji hawa - Andrew Kibe

“Rais mchunge mkewe kutokana na wachungaji hao wanafiki. Hao wachungaji watatuharibu si watu wazuri" - Andrew Kibe

image
na Radio Jambo

Burudani16 September 2022 - 11:55

Muhtasari


• Mwambie mkewe kuzingatia katika kukuhudumia na wewe kuzingatia katika kuendesha nchi - Kibe

Kibe amtaka Ruto kumlinda mkewe dhidi ya wachungaji

Siku chache baada ya kuapishwa kwa Ruto kama rasi wa tano, kumekuwa naminong’ono mingi mitandani kuhusu jinsi rais huyo na mkewe wanavyojiweka kwa njia ya Kikristu.

Jana msanii mkongwe wa injili na aliyekuwa mgombea urais kabla ya IEBC kumfungia nje, Reuben Kigame alizua mjadala Twitter akidai kwamba serikali ya Ruto inatumia Biblia na ucha Mungu vibaya.

Wengi waliachwa vinywa wazi na matamshi haya kutoka kwa mwinjilisti huyo, hay ani baada ya mama taifa Rachael Ruto kuwakaribisha watumishi wa Mungu mbalimbali katika ikulu ya Nairobi.

Watu wamekuwa wakigawanyika kuhusu mjadala huo huku wengine wakisema Ruto na mama taifa hawafai kukaribisha machungaji na wahubiri katika ikulu huku wengine wakisema ni sawa kwani ndio hatua nzuri ya kuonesha nchi kuwa ya wachamungu kutoka kwa kiongozi wa taifa.

Mwanablogu Andrew Kibe naye hajaachwa nyuma katika kulitilia suala hilo kweney mizani. Kupitia YouTube yake, Kibe alimtaka rais William Ruto kumlinda mkewe kutoka kwa wachungaji hawa wote wanaotaka kukutana naye kweney ikulu kwani wengine ni jina na umaarufu tu wanataka kujizolea kupitia jina la mama Rachael na ikulu kwa ujumla.

“Rais mchunge mkewe kutokana na wachungaji hao wanafiki. Hao wachungaji watatuharibu si watu wazuri. Baadhi yao ni watu wabaya sana, mwambie mkewe kuzingatia katika kukuhudumia na wewe kuzingatia katika kuendesha nchi, hayo mengine ni ya uongo,” Andrew Kibe alisema.

Kulingana na Kibe, aliwataka viongozi kuwaweka wake zao mbali na uongozi haswa wa taifa na wakome kuwaweka kwenye mwanga wa kushughulika na masuala ya uongozi kwa kile alisema wananchi walimchagua yeye na si mkewe.

Juzi mama Rachael kupitia kwenye Twitter yake alidokeza kwamba aliwapokea na kuwakaribisha wachungaji katika ikulu ya Nairobi, siku chache tu baada ya kuhamia ikuluni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved