logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rotimi hatimaye afunguka sababu ya kuchumbiana na Vanessa Mdee

Rotimi alisema kando na Vanessa kuwa mrembo, pia anajua jinsi na wakati wa kuwa shupavu.

image
na Radio Jambo

Habari30 September 2022 - 04:25

Muhtasari


•Rotimi anachumbiana na mwimbaji wa Tanzania Vanessa Mdee na wako na mtoto mmoja wa kiume pamoja.

•Rotimi aliwataja wanawake wa Kiafrika kuwa wanyenyekevu.

Muigizaji wa Nigeria anayeishi Marekani Olurotimi Akinosho almaarufu Rotimi ameeleza kwanini yuko kwenye mahusiano na mwanamke wa Kiafrika.

Rotimi anachumbiana na mwimbaji wa Tanzania Vanessa Mdee na wako na mtoto mmoja wa kiume pamoja.

Akizungumza katika mahojiano na The Pivot Podcast, Rotimi aliwataja wanawake wa Kiafrika kuwa wanyenyekevu.

"Unapokuwa na mwanamke wa Kiafrika, unapata mwanamke ambaye ni makini kuhusu tunavyoelewa jinsi ya kumtendea mwanaume na jinsi ya kunyenyekea," alisema.

Rotimi alisema kando na Vanessa kuwa mrembo, pia anajua jinsi na wakati wa kuwa shupavu.

"Ni usawa tu ambao ni vigumu kuupata na sisemi kuwa haupati hivyo kwa wanawake wa Marekani, lakini wanawake wengi wa Kiafrika wamefanywa kuwa malkia katika akili zao na pia kuwa wake wazuri."

Mnamo Septemba 28, wanandoa hao walisherehekea siku ya kuzaliwa ya mtoto wao Seven.

Vanessa alimmwagia sifa kochokocho mwanawe huku akimshukuru Mungu kwa kumjalia mtoto wa kiume.

"Mtoto wangu, wewe ni zawadi ya kimungu na ninaheshimiwa kuwa Mama yako. Asante kwa kuwa baraka yetu kuu," aliandika.

Rotimi pia alimtaja mkewe kama mwanamke mwenye nguvu.

Wanandoa hao wanadaiwa kupanga kufanya harusi ya Kizungu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved