logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jinsi upasuaji wangu wa matiti ulihasisha watu - Vera Sidika

Sidika alisema kuwa upasuaji wake uliwahamasisha watu wengi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri14 October 2022 - 07:13

Muhtasari


• Alisema kuwa sasa hivi watu wengi haswa wanawake huwa hawaongelei upasuaji huo mabaya  na kuwa wameweza kuiona kama njia nzuri ya kubadlisha umbo.

• Aliongeza kuwa upasuaji huo uliwasaidia wanawake wanaougua ugonjwa wa Saratani ya matiti na kuwatolea hofu ya kukemewa na watu.

Vera Sidika alieleza jinsi umbo lake na upasuaji wake wa makalio umewaelemisha watu.

Alisema kuwa upasuaji huo aliufanya wakati watu bado hawakuwa wamefahamu kuwa kuna mchakato wa kuongeza viungo vya mwili.

Licha ya kukemewa alipoonekana mara ya kwanza akiwa na umbo hilo lake, watu waliweza kujua kuwa kuna uwezo wa kuukarabatisha mwili wao.

"Kitu kimoja ninachoweza kusema ni kuwa nilielimisha watu watu wengi kuhusu upasuaji huu wa kimaumbo wakati na sasa karibu kila mtu anaufanya".

Alisema kuwa sasa hivi watu wengi haswa wanawake huwa hawaongelei upasuaji huo kwa ubaya  na kuwa wameweza kuiona kama njia nzuri ya kubadlisha umbo.

Hata hivyo, Sidika alisema kuwa wanawake wengine wamehamasishwa na marafiki zao kufanya upasuaji huo na kuutumia vibaya.

Mama huyo wa mtoto mmoja aliongeza kuwa baadhi ya watu wanatumia upasuaj huo kwa njia isiyo faa na wanaweza kukutwa na madhara mbalimbali.

"Watu wengi waliohamasihwa kuufanya upasuaji huo hawajui madhara yake, unapata mtu anafanya upasuaji huo anafariki akiwa kwenye mchakato huo ama baadaye anabadilika kabisa," Sidika alisema.

Aliongeza kuwa upasuaji huo uliwasaidia wanawake wanaougua ugonjwa wa Saratani ya matiti na kuwatolea hofu ya kukemewa na watu.

"Upasuaji huu ulipotokea ulikuwa kwa ajili ya kuzuia huzuni miongoni mwa wanawake ambao wamekuwa na saratani ya matiti na ni mchakato ambao ni bora kabisa," mwanansosholaiti huyo aliwafahamisha watu.

Sidika alisema sababu yake ya kufanyiwa upasuaji huo ni kuwa alihisi mwili wake haukua na usawa, alikuwa amebarikiwa na makalio ila matiti yalikuwa madogo.

Aliongeza kuwa mtu akiwa na umbo zuri hawezi kuwa na tashwishi yoyote na umbo lake na kuwa hawezi kushinikizwa kujibalisha.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved