logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Betty Kyallo azama tena kwenye dimbwi la mahaba

Hivi majuzi Nick alisema anampeza mpenzi wake wa zamani, akimtaja kama mtu mzuri.

image
na Radio Jambo

Makala31 October 2022 - 03:55

Muhtasari


•Betty alichapisha picha yake akiwa ameshikilia shada la maua, na kusema hilo ndilo tukio maalum la wiki yake.

•Hivi majuzi Nick alisema anampeza mpenzi wake wa zamani, akimtaja kama mtu mzuri.

Mtangazaji na mjasiriamali maarufu Betty Kyallo amedokeza kuhusu kuwa mahusiano mapya.

Hivi majuzi, mama huyo wa mtoto mmoja alichapisha picha yake akiwa ameshikilia shada la maua, na kusema hilo ndilo tukio maalum la wiki yake.

"Mapenzi ni kitu kizuri," aliandika.

Mahusiano ya mwisho ya hadharani ya Betty Kyallo yalikuwa na wakili Nick Ndeda.

Wawili hao walipoachana, Betty alisema walikuwa na mitazamo tofauti ya masuala fulani ya kimaisha.

"Katika mahusiano, ni kuhusu kufahamiana. Ilifika mahali ambapo tulikuwa hatuna mwelekeo sawa upande na uhusiano."

Hivi majuzi Nick alisema anampeza mpenzi wake wa zamani, akimtaja kama mtu mzuri.

"Ninakosa mambo fulani fulani, sitasema uwongo. Nishati nzuri na yote," Nick alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved