logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Walinitumia kisha wakanitupa!" Mzee wa kutangaza habari za vifo alia

Mzee Geoffrey Jjemba Matte aligonga vichwa vya habari kutokana na staili ya kipekee ya kutangaza mazishi.

image
na Davis Ojiambo

Burudani31 October 2022 - 13:26

Muhtasari


  • • Mzee huyo alisema sasa amelazimika kurejelea shughuli zake za ukulima baada ya watu wote kumtelekeza baada ya kumtumia vibaya.
Mzee wa kutangaza habari za vifo

Kwa wapenzi wa mitandao ya kijamii, bila shaka mtakuwa mmeiona picha ya  mzee mmoja ambaye alisemekana kuwa raia wa Uganda.

Mzee huyo ambaye picha yake akionekana kutangaza katika hafla ambayo wengi waliamini ni mazishi akiwa ameshikilia karatasi nyingi kwa mkono mmoja huku mkono mwingine ameshika kipaza sauti, picha hiyo ilisambazwa sana na hata wengi kuitumia kama kichekesho – meme.

Kulingana na jarida la Daily Monitor nchini Uganda, liliripoti kuwa mzee huyo kwa jina Godfrey Jjemba Matte, amerudi katika shughuli zake za kilimo baada ya kuripotiwa "kutumiwa na kutupwa na wanasiasa na watu mashuhuri."

Mzee huyo mwenye umri wa miaka 69, alijikuta akitrend kwenye mtandao na hivyo kumfanya kuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii inayotumika sana huku picha na katuni zikichorwa kutokana na mtindo wake wa kipekee wa kusoma matangazo ya mazishi.

Pia alipokea ahadi kama redio ya jamii, pikipiki na miwani ya dirisha na milango, ambayo anasema haijawahi kutimizwa.

“Watu bado wananiita mtu mashuhuri lakini nimerejea kwenye kilimo kwa sababu baadhi ya watu walikuja hapa na kunitumia kwa maslahi yao binafsi kisha kunitelekeza. Kuna mchungaji mashuhuri anayeishi Kampala ambaye aliahidi kunipa viunzi vya madirisha na vioo kwa ajili ya nyumba yangu mpya lakini bado hajatimiza ahadi hiyo. Unaweza kuona jinsi mtu wanayemwita mtu mashuhuri anavyolala,” jarida hilo lilimnukuu mzee Jjemba aliyeonekana kuchanganyikiwa.

Jjemba aliyekasirishwa pia alifichua kwamba aliacha kutoa mahojiano "ya bure" kwa waandishi wa habari kwa sababu hapati chochote kutoka kwa mahojiano.

Baba huyo wa watoto 11 alisema baadhi ya mali za nyumbani alizochangiwa, runinga ya aina yake iliibiwa hivi majuzi na majambazi waliovamia nyumbani kwake usiku.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved