logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kwa nini Diamond hawezi kufikia kiwango cha Burna Boy- MCA Tricky afichua

Tricky amebainisha kuwa ni ngumu kwa wasanii wa Afrika Mashariki kufika kimataifa katika mazingira ya sasa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri02 November 2022 - 04:31

Muhtasari


•Tricky alidokeza kuwa tatizo kubwa linalowakabili wanamuziki wa Kenya na wa Tanzania ni kikwazo cha lugha.

•Alisema suala la kizuizi cha lugha linapaswa kushughulikiwa haraka sana ili kusukuma muziki wetu mbali zaidi.

Mchekeshaji Francis Munyao almaarufu MCA Tricky amebainisha kuwa si rahisi kwa wasanii wa Afrika Mashariki kufika kimataifa katika mazingira ya sasa.

Katika mahojiano na Mpasho, Tricky alidokeza kuwa tatizo kubwa linalowakabili wanamuziki wa Kenya na wa Tanzania ni kikwazo cha lugha.

Alisema lugha ya Kiswahili ambayo hutumiwa sana na wasanii wa nchi hizo mbili za Afrika Mashariki imewazuia kufikia viwango vya kimataifa.

"Wale wasanii tuko nao hapa Kenya wana talanta kubwa hata kuliko Wanigeria hawa wanafurika hapa. Chanzo kikuu cha tatizo ni kikwazo  cha lugha. Kwa nini Wanigeria hawachezi ngoma za Otile Brown, ni kwa sababu 80% ya ngoma zake ni Kiswahili. Hawaelewi Kiswahili watacheza vipi ngoma za Otile Brown," alisema.

Mchekeshaji huyo pia alidokeza kuwa Diamond Platnumz licha ya kipaji chake na jina kubwa alilonalo katika ukanda wa Afrika Mashariki ameshindwa kufika viwango vya juu kwa sababu ya kikwazo cha lugha.

"Ni kwa nini Diamond hawezi kufika viwango vya kina Burna Boy? Ni kwa sababu 80% ya nyimbo zake ni Kiswahili. Watu wanafurahia midundo tu lakini wanang'ang'ana kusikia. Kikwazo cha lugha ni tatizo kubwa," alisema.

Alisema suala la kizuizi cha lugha linapaswa kushughulikiwa haraka sana ili kusukuma muziki wa Afrika Mashariki kuenda mbali zaidi.

"Wacha tukuze utamaduni wa kuungana na ulimwengu kwa haraka kwa kujifundisha Kiingereza au Kichina," alisema.

Aidha, mchekeshaji huyo alipongeza juhudi za mchekeshaji mwenzake Eric Omondi kusukuma muziki wa Kenya kuchezwa zaidi.

Hata hivyo alibainisha kuwa wazo la Eric, licha ya kuwa nzuri,jinsi ya kulitekeleza haijafikiriwa vizuri na mengi yanaweza kufanywa kulifanikisha hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved