logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Eric Omondi ampoteza mwanawe,amuomboleza kwa ujumbe wenye hisia

Katika video hiyo tulimwona Lynne akihangaika na anaonekana kuwa na maumivu.

image
na Radio Jambo

Habari08 November 2022 - 14:39

Muhtasari


  • Eric Omondi ampoteza mwanawe,amuomboleza kwa ujumbe wenye hisia
  • Alisema hawakuwahi kukutana lakini watampenda milele

Mchekeshaji maarufu Eric Omondi kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amefichua kwamba mpenzi wake Lynne alipoteza ujauzito wake usiku wa kuamkia leo.

Kwenye chapisho la hisia na mchekeshaji mtata Eric ameomboleza mtoto wao akisema kwamba walijitolea kwa zaidi ya masaa 5 lakini Mungu alikuwa na mipango mingine.

Katika video hiyo tulimwona Lynne akihangaika na anaonekana kuwa na maumivu. Eric Omondi pia anaonekana kujaribu kumfariji.

Eric Omondi alinukuu kuwa usiku wa jana ulikuwa mojawapo ya usiku mrefu zaidi maishani mwake.

Alisema hawakuwahi kukutana lakini watampenda milele.

"Usiku wa jana ulikuwa mojawapo ya usiku mrefu zaidi maishani mwangu. Tulipigana kwa zaidi ya saa 5 kujaribu kuokoa malaika wetu mdogo lakini Mungu alikuwa na mipango mingine. Hatukuwahi kukutana lakini hakika tulikuhisi na tutakupenda milele. Heshima kwa wanawake wote hakuna mwanaume duniani mwenye nguvu za aina hiyo @lynne stay strong it is well."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved