logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jovial aahirisha kutoa kibao kipya baada ya kuugua

Jovial ana sababu ya kumshukuru Mungu kwa kuokoa maisha yake.

image
na Radio Jambo

Burudani10 November 2022 - 11:15

Muhtasari


  • Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram msanii huyo alifichua kwamba kama timu yake haingekuwa naye hajui mahali angekuwa

Msanii Jovial atachukua muda wa mapumziko kutoka kwa mitandao ya kijamii baada ya kuanguka.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram msanii huyo alifichua kwamba kama timu yake haingekuwa naye hajui mahali angekuwa.

Kulingana na msanii huyo, alikuwa anatarajia kutoa kibao wiki hii, lakini hataweza kwani hayuko kwenye hali ya kutoa kibao.

Jovial ana sababu ya kumshukuru Mungu kwa kuokoa maisha yake.

"Mwili yangu imekataa leo ile kuanguka nimeanguka kama ningekuwa  pekeyangu sijui ingekuwa aje, jana nilikuwa naambia timu yangu kimchezo kwwamba sihisi vizuri lakini nitakuwa sawa

Hivi ndivyo watu hufariki, leo wako sawa na kesho wameenda,niruhusu nipumzike nilikuwa niachie kibao kipya lakini nitaihirisha mpaka wiki ijayo,ikiwezekana nitaweza aachia vibao mara mbili

Sitakuwa kwenye mitandao ya kijamii,"Aliandika Jovial.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved