logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wasanii wa Tanzania tunatumia Muda Mwingi Kushindana na Kupigana Vijembe-Diamond

Aliongeza kuwa kabla ya kuimba huwa anazungumza na Mungu ili amuongoze kwa njia ipasavyo.

image
na Radio Jambo

Burudani24 November 2022 - 09:53

Muhtasari


  • Diamond akizungumza akiwa kwenye harambee msikitini alisema kwamba wasanii wamekuwa wakitumia muda wao mwingi kupigana vijembe

Naseeb Abdul anayefahamika kwa jina la kisanii Diamond Platnumz na ambaye anafuatiliwa sana kwa ukaribu na mashabiki wake amewasihi wasanii wa Tanzania waache kushandana wenyewe kwa wenyewe.

Diamond akizungumza akiwa kwenye harambee msikitini alisema kwamba wasanii wamekuwa wakitumia muda wao mwingi kupigana vijembe.

Aidha msanii huyo alisema kwamba wasanii hao wanapaswa kushindana na wasanii kutoka nchi zingine kama vile Nigeria.

"TUACHE KUSHINDANA WENYEWE, TUSHINDANE NA WA-NIGERIA,Wasanii wa Tanzania tunatumia Muda Mwingi Kushindana na Kupigana Vijembe kwa vitu visivyo namsingi, Wakati Wenzetu wa Magharibi (Nigeria) Wanazidi kupiga hatua. Tuache Kushindana Wenyewe," Diamond platnumz alisema.

Pia alisema kwamba uhusiano wake na Mungu uko sawa na imara , kwani watu wamekuwa wakichanganya uimbaji wake na uhusiano wake na Mungu.

Aliongeza kuwa kabla ya kuimba huwa anazungumza na Mungu ili amuongoze kwa njia ipasavyo.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved