logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize kutumia wimbo kueleza mapenzi yake kwa bangi

Staa huyo wa Bongo pia ametangaza kuwa ataanza kutoza Ksh 5M ili kufanya collabo na wasanii wengine.

image
na Radio Jambo

Burudani01 December 2022 - 05:46

Muhtasari


•Harmonize ameapa kuachia wimbo unaohusu mihadarati hiyo haramu katika nchini  Tanzania kabla ya mwisho wa mwezi wa Disemba.

• Pia ametangaza kuwa ataanza kutoza Ksh 5M ili kufanya  collabo na wasanii wengine.

Staa wa Bongo Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize ameapa kutunga wimbo kuhusu mmea wa Bangi.

Harmonize ambaye kwa muda mrefu amekuwa wazi kuhusu mapenzi yake kwa bangi ameahidi kuachia wimbo unaohusu mihadarati hiyo haramu katika nchini mwake Tanzania kabla ya mwisho wa mwezi wa Disemba.

"Disemba hii, nisipotengeneza wimbo kuhusu bangi .. nipigeni risasi," alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Aliambatanisha ujumbe wake na emoji ya kikohozi, ambacho huwa anatumia kama utambulisho wake katika nyimbo zake nyingi. Kikohozi pia huhusishwa na matumizi ya bangi kwani watumizi wengi hujipata wakikohoa baada ya kuvuta.

Konde Boy kwa kawaida huwa hafichi kwamba yeye ni mtumizi wa mihadarati hiyo. Katika video za nyimbo zake nyingi ameonekana akivuta kinachoaminika kuwa bangi. Pia amewahi kurekodi video zingine nyingi akivuta.

Bosi huyo wa Konde Music Worldwide pia ametangaza kuwa ataanza kutoza Ksh 5M ili kufanya  collabo na wasanii wengine.

"Naanza kutoza kwa collabo, TZS 100M. Sharti ngoma iwe kali. Siwezi kusubiri kumtoza mtu fulani TZS 500," alisema.

Mapema mwaka huu, Konde Boy alidokeza kuhusu mpango wake wa kuanzisha Brand ya sigara. Staa huyo alituma ombi kwa mabwenyenye wa Tanzania kujitolea kushirikiana naye kufanikisha ndoto ya kuanzisha kampuni ya kutengeneza sigara.

Katika taarifa yake, Harmonize alisema kuwa anatafuta mshirika ambaye yupo tayari kuwekeza naye huku akidai ni wengi wanaoisubiri bidhaa yake kwa hamu.

"Nataka mtu ambaye atawekeza vizuri. Tufanye hili pamoja. Hakuna haja ya kufanya hili pekee yangu. Nahitaji ushirikiano mkubwa. Kila mtu anajua kiasi gani mtaa unasubiri hii kitu kwa hamu," Harmonize alitangaza.

Bosi huyo wa Konde Music Worldwide alifichua kuwa bidhaa yake itatambulika kama sigara ya Tembo. Alisema kuwa kampuni yake itatengeneza sigara kwa kutumia  tubaku inayolimwa nchini Tanzania.

Tembo cigarrette, tobako linalolimwa hapa hapa Tanzania!! Haya sasa matajiri waingie. Wachina sisi wenyewe tunaweza. Bei mtajipangia wenyewe wanangu," Alisema.

Mwanamuziki huyo aliwataka washirika watakaovutiwa na pendekezo kuwasiliana na wasimamizi wake Chopa , Dkt Sebastian Ndege na Mohamed Mmari almaarufu Mjerumani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved