logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mkeo ni mimi nilimpa nguo unaona akivaa - Sonko amnyamazisha mnoko wa mtandaoni (screenshot)

Jamaa huyo alijaribu kujua kwa nini chumba cha Sonko kilikuwa na viatu vingi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri10 December 2022 - 10:10

Muhtasari


• Sonko alikuwa amepakia picha akiwa na msanii Lavalava kwenye ofisi yake wakikagua rafu ya viatu.

Sonko akimkomesha jamaa mnoko

Katika siku za hivi karibuni, watu maarufu wamekuwa wakipitia wakati mgumu mitandaoni kutokana na kuburuzwa na wanamitandao kwa kashfa mbalimbali.

Lakini unaambiwa siku zote hakuna swali lisilo na jibu. Watu maarufu nao wamepata njia mbadala ya kuzima masimango kwa kujibu mipigo ifaavyo bila kujali nini mashabiki na wafuasi wao watawafikiria.

Juzi aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko alipakia rundo la picha kwenye ukurasa wake wa Facebook akiwa na msanii wa Tanzania, Lavalava. Lava alikuwa amemtembelea Sonko katika ofisi yake jijini Nairobi kutokana na maelezo kwenye picha hizo zaidi ya 20.

“Jana msanii nguli Lavalava kutoka Tanzania alinitembelea katika ofisi zangu Upper Hill Nairobi,” Mike Sonko aliandika.

Kwenye sehemu ya kutoa maoni, mtumizi mmoja wa Facebook aliyetaka kujua kama kweli hiyo ni ofisi ya Sonko ama ni duka lake la kuuza viatu, alipata jibu zito kutoka kwa Sonko.

Kuchora picha kamili, Sonko na Lavalava walionekana wakitizama rafu zilizokuwa zimejazwa viatu, jambo lililozua maoni tofauti kutoka kwa baadhi ambao walishindwa kuelewa kama ni duka ama ni ofisini mwaka kama alivyoelezea kwenye kapsheni.

Kwa utani mwingi, Sonko alimpiga kumbo mtu huyo kwa jina Kilonzo Dhe Shaddie kwa kumtania kuwa hata nguo na viatu vya mkewe ni yeye mwenyewe alimpa.

“Hata zile kanda mbili za mkeo na ile bikini, sketi ya bluu ukiongeza na suruali nyekundu unazomuona akivaa ni mimi nilimpa,” Sonko alijibu bila huruma wala kusita.

Jibu hili lilivutia vichekesho kutoka kwa watu baadhi wakisema ndio njia ya pekee kumjibu mtu anayejaribu kudadisi mambo yako ya faragha huku wengine walimsuta Sonko kuwa aliyeuliza hakuwa na ubaya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved