logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize ajibu madai ya kumcheza kajala na video Vixen wake

“Sijui wewe!! Acha kumzungumzia kaka yako aliyesaidia kutimiza ndoto zako, niheshimu.

image
na Radio Jambo

Habari29 December 2022 - 11:57

Muhtasari


  • Hata hivyo alisema anafurahi kuwa Harmonize na aliyekuwa mpenzi wake Fridah Kajala wameachana na kumuomba Harmonize kutafuta msichana wa aina yake

Mwimbaji kutoka Tanzania Harmonize amekana kuwa na uhusiano wa kimapenzi na video vixen wa video yake ya ‘Amelowa’.

Harmonize aliyekasirika alimkashifu vikali mwanamke huyo aliyetambulika kwa jina la Sophie akisema hawajawahi kukutana baada ya kurekodi video.

Mkali huyo wa 'Uno' alimtaja vixen kuwa mtu asiye na shukrani ambaye hakuthamini nafasi aliyompa ili kutimiza ndoto zake.

“Sijui wewe!! Acha kumzungumzia kaka yako aliyesaidia kutimiza ndoto zako, niheshimu.

Hujawahi kuniona baada ya video, hili ndilo tatizo la kuwa mnyenyekevu, unawapa watu fursa na wanafikiri ni sawa na wewe,” aliandika Harmonize kwenye stori zake za Instagram.

Katika mahojiano na vyombo vya habari vya Tanzania, Sophie hata hivyo alikanusha kuwa na uhusiano wowote na nyota huyo akisema uvumi huo pia ulimpata bila kufahamu.

Hata hivyo alisema anafurahi kuwa Harmonize na aliyekuwa mpenzi wake Fridah Kajala wameachana na kumuomba Harmonize kutafuta msichana wa aina yake.

“Mara ya mwisho kuongea na Harmonize ni wakati wa kushoot video, hatujawasiliana tangu wakati huo, amekuwa bize na mambo yake na mimi nimekuwa bize na zangu.

"Hata hivyo nilifurahi kwamba aliachana na Kajala na sijali kuchukua nafasi yake ikiwa Harmonize anataka hivyo," Sophie alisema.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved